Header Ads

Breaking News
recent

MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA ZASABABISHA MFUMKO WA BEI ZA MATUNDA MKOANI MOROGORO.


Image result for picha za matunda

21 APRIL  2018         MOROGORO           BIASHARA
Mwenyekiti wa soko la Mawenzi Manispaa ya Morogoro  Ramadhani  Mohamedi,  ametoa ufafanuzi juu ya hali ya Biashara ya Matunda  hasa katika kipindi hiki cha Mvua zinazoendelea kunyesha mkoani hapa.
Mohamedi amesema kuwa,  kuna baadhi  ya bidhaa ambazo zimepanda bei hususani vitunguu na Nyanya kutokana na hali ngumu ya usafirishaji wa bidhaa hizo  kutoka mashambani hadi sokoni hali inayosababisha bidhaa hizo kuoza.
“Matunda niseme pia msimu bado haujachanganya lakini mvua nazo zinachangia kwasababu usafirishaji wa matunda kutoka mashambani unategemea magari na barabara kwa sasa ivi barabara zimekuwa sio nzuri na matunda yakifika sokoni yakiwa yameharibika inasababisha bei kuuzwa kubwa”
Aidha Mfanyabiashara wa matunda katika soko hilo Imani mhawi,  amesema kuwa msimu huu wa mvua zinazoendelea kunyesha imesababisha bei za matunda kupanda kwa kasi, pia wamekuwa na changamoto ya  wanunuzi wengi kushindwa kufika sokoni kwa wakati.
“Changamoto tunazokutana nazo ni usafirishaji kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha na matunda kutoka kule shambani mpaka yafike sokoni yanakuwa yameharibika”

No comments:

Powered by Blogger.