Header Ads

Breaking News
recent

NJIA TATU (3) PEKEE ZA KUKUZA BIASHARA


1. Ongeza Idadi Ya Wateja.

Nafikiria unafahamu kuwa wateja ndio wanaokuingizia pesa katika biashara yako.Na kila ukiwa na wateja wengi ndivyo kipato kinavyozidi.Na kila wanavopungua ndivyo kipato kinapungua na hatimae kuuwa biashara yako.

Je Wateja Wako Utawapata Wapi?

Wateja hawapatikani isipokuwa wewe (au hata watu wengine) kutangaza kwa watu kuwa una biashara fulani yenye kutoa bidhaa au huduma fulani.Na njia kuu ya kupata wateja ni kutangaza.Na matangazo unaweza kufanya kwa njia mbili.
1.      BURE – Kuwa na duka au ofisi sehemu iliyo mbele za nyuso za watu, kuongea na watu ana kwa ana, kutumia mitandao ya kijamii n.k
2.      Kulipia matangazo – Hii itakusaidia kuwafikia maelfu ya watu kwa mpigo kitu ambacho kitakusaidia kuongeza idadi ya wateja wapya mara moja.
2. Ongeza Idadi Ya Mauzo Ya Kila Mteja.
Kama kila mteja anakuingizia wastani wa shilingi elfu kumi kwa kila manunuzi, inabidi ujitahidi kumshawishi mteja huyo kununua bidhaa za ziada zitakazokufanya uongeza mapato kwa kila manunuzi.Swala la kujiuliza ni bidhaa gani ya ziada unayoweza kuwauzia wateja wako juu ya kile kitu wanachonunua  kila siku.
Mfano biashara ya hoteli umepewa  oda ya burger, wanakuuliza “je utapenda tukuwekee na chipsi katika hiyo burger?” ukisema ndio wanakuuliza tena “utapenda tukuwekee na kinywaji gani?”Wewe na yako ilikuwa ni burger pekee yake lakini umejikuta unanunua na chipsi na soda.
3. Ongeza Idadi Ya Mauzo Endelevu.
Jambo la tatu la muhimu kufanya ni kuhakikisha wateja wako wanarudi kwako mara kwa mara kununua bidhaa au huduma unayotoa.Unaweza kufanya hivi kwa:
1.      Kuuza bidhaa au huduma inayopendwa na wateja wako
2.      Kuwasiliana na wateja wako mara kwa mara kuwajulisha kuhusu OFA au bidhaa au huduma mpya ambazo umezileta kwa wakati huo.

No comments:

Powered by Blogger.