Header Ads

Breaking News
recent

Namna ya kulisha kuku Ili wasipatwe na magonjwa


Image result for picha ya kuku
Ili uweze kuepusha magonjwa kwa kuku zingatia mambo haya yafuatayo:
      Safisha vyombo vya kulishia na kunyweshea kila siku. Osha, sugua vizuri, kisha suuza kuondoa utando unaobeba bakteria.
      Kuku wanahitaji wapewe chakula cha kutosha na chenye virutubisho vyote. Unaweza kuwaongezea majani, makombo, nafaka, mchanga laini, au maganda ya mayai.
    Wapatie kuku maji safi muda wote. Wafugaji wengi wameripoti kuwa na matokeo mazuri baada ya kuchanganya dawa ya kuua vimelea kwenye maji ya kunywa.
   Nunua chakula kwa wauzaji wazuri na wanaoaminika ili kuepuka minyoo na sumu hatarishi. Usiwape kuku chakula chochote kinachoonekana kuoza au kunuka uvundo.
   Hifadhi chakula cha kuku katika sehemu kavu isiyo na joto na isiwe kwa zaidi ya miezi mitatu ili kuepuka kuharibiwa na fangasi.
Kwa taarifa zaidi ntafte kwa namba watsap  0719257061 au kupitia email yangu zuhuraamani24@gmail.com

No comments:

Powered by Blogger.