SOMA JINSI YA KUFANYA BIASHARA KWA WELEDI SANA
UJASIRIAMALI NI MUHIMU KWA MAENDELEO ENDELEVU TANZANIA.
Nini maana ya Ujasiriamali na Mjasiriamali?
Mjasirimali ni yule mtu anayegundua au
anayeboreasha wazo la biashara.
Ujasiriamali ni kile
kitendo cha kubuni au kuboresha wazo la biashara na kulifanyia kazi ya aidha
kuuza bidhaa au kutoa huduma. Kwenye hili, mtu anakua na wazo ambalo anataka
kulifanyia kazi ili apate faida baada ya kulitekeleza.
SIFA ZA MJASIRIAMALI
kuna sifa za jumla ambazo wajasiriamali wengi huwa nazo. Sifa hizo
ni kama zifuatazo:
i.Ubunifu
Hii ni moja ya sifa ambazo mjasiriamali ni lazima awe nazo. Mbunifu ni yule mtu mwenye uwezo wa kuja na mawazo ya kuwa na huduma au biashara mpya inayohitajika sokoni. Kuwa mbunifu haimaanishi kuwa mtu anakuja na mawazo mapya kila mara, ila inaweza kuwa ni uwezo wa kuja na mbinu au njia mpya za kutengeneza, kuuza au kutangaza bidhaaa au huduma ambayo tayari ipo.
Hii ni moja ya sifa ambazo mjasiriamali ni lazima awe nazo. Mbunifu ni yule mtu mwenye uwezo wa kuja na mawazo ya kuwa na huduma au biashara mpya inayohitajika sokoni. Kuwa mbunifu haimaanishi kuwa mtu anakuja na mawazo mapya kila mara, ila inaweza kuwa ni uwezo wa kuja na mbinu au njia mpya za kutengeneza, kuuza au kutangaza bidhaaa au huduma ambayo tayari ipo.
ii.Kuwa mtu
wa kushikilia na kuhangaikia kukamilisha malengo unayojiwekea
Mtu
mwenye malengo ni yule mtu ambae anashikilia nakukazania malengo ambayo
amejiwekea. hii ni sifa nyingine ya mjasiriamali mzuri, kwa maana kama
hautajiwekea na kushikilia malengo yako binafsi ni rahisi sana kuyumbishwa na
matatizo madogo madogo yanayoweza ikumba biashara yako. Lakini ukiwa na malengo
thabiti, nirahisi kuwa na jibu kwenye kila tatizo unalopata.
iii.
Kujiamini
Mara
nyingi kujiamini huja baada ya kuwa na malengo thabiti ukishakuwa na malengo
thabiti kinachofuata ni kuamini mipango yako italipa. Kujiamini ni muhimu kwa
sababu kuna kupa nguvu ya kukabiliana na vikwazo vinavyoweza kuiikumba biashara
yako.
iv.
Kufanyakazi kwa Juhudi
Cha
mwisho, mjasiriamali ni lazima afanye kazi kwa bidii. Kufanyakazi kwa bidii
haimaanishi mjasiriamali afanye kazi zote yeye mwenyewe, inamaanisha awe tayari
kupunguza mambo mengine na kuwekeza muda mwingi kwenye biashara yake. Mara
nyingi, kuwa mjasiriamali kunamaanisha wewe ndio bosi wa biashara yako, hivyo
nilazima uwe na nidhamu ya kujisimamia na kusimamia watu wengine wanaokusaidia
katika biashara yako.
Mteja ni nani?
Mteja
ni mtu au tasisi yoyote ambaye una uhusiano naye katika biashara. Si lazima
mteja awe ni yule anayenunua bidhaa au huduma kutoka katika biashara yako leo.
Hata
yule mtu anayekuja kuulizia au kutembelea biashara yako ni mteja vilevile.
Vidokezo vya kujenga uhusiano
mwema na wateja.
Kila
mara msalimie mteja na kisha muulize “ Naweza kukusaidia”?
Kwanza
jifunze kuwa msikilizaji mzuri. Sikiliza na kuelewa.
Kama
hujaelewa, uliza ili kukidhi haja ya mteja.
Kuwa
mkarimu kwa wateja wote. Wahudumie kwa tabasamu. Watimizie wanachotaka kwa utaratibu
ulio wazi.
Wahudumie
wateja kwa makini.
Ruhusu
wateja wazijaribu bidhaa zako (inapobidi).
Kubali
malalamiko na ujibu kwa uangalifu.
Zungumza
kidogo, onyesha zaidi.
Uza
manufaa, siyo bidhaa pekee.
Kila
mara jaribu kuwa na subira, kwasababu wateja wengine ni wazito kuamua.
Mambo Yasiyofaa
Usibishane
na mteja
Usimchanganye
mteja kwa maelezo mengi mno.
Usimuuzie
mteja zaidi ya kile anachoweza kutumia
Usikate
tamaa mteja anaposema kwamba bei ni kubwa mno. Badala yake mweleze manufaa
atakayopata
Usimlazimishe
mteja kununua, bali mshawishi.
Usimkatize
mteja anapozungumza, yeye ndiye mfalme.
Usinywe,
usivute, wala usile unapokuwa unauza, hivi ni vitendo vinavyoweza kumkera mteja.
Mambo ambayo huweza kuharibu
uhusiano na mteja
Uso
wenye hasira
Uso
unaoonyeha kusononeka au kuchoka.
Kutojali
mteja anapokuja
Kutoa
huduma kwa upendeleo
Kuonyesha
kutokuwa na ujuzi katika utoaji huduma
Kutoa
huduma pole pole sana
Lugha
isiyofaa
Kukejeli
wateja
Kumdai
mteja kitu kilicho nje ya utaratibu ndipo huduma itolewe
Kutotekeleza
ahadi
Kupokea
zawadi kutoka kwa wateja (zenye nia ya kutoa upendeleo)
Kujenga
mahusiano ya kimapenzi na wateja
Kutowatimizia
wateja mahitaji yao
Kupiga
soga wakati wateja wanasubiri
Kutoa
huduma huku umelewa.
Kushindwa
kutoa faraja kwa wateja wakati inapobidi wasubiri huduma
Kwa fundisho zaidi tembelea ukrasa wangu wa facebook (zuhura
Amani) na tweter (Zuhura Aman) watsap (0719257061) email. zuhuraamani24@gmail.com.
No comments: