Header Ads

Breaking News
recent


USIMAMIZI WA RUTUBA YA UDONGO KATIKA KUONGEZA UZALISHAJI WA MAZAO



RUTUBA YA UDONGO

 Rutuba ya udongo ni nini?

 Rutuba ya udongo inafafanuliwa kwa uwezo wake wa kutoa virutubisho vyote muhimu kwa kiasi kinachotosheleza na katika urari sahihi kwa ajili ya ukuaji wa mimea, bila ya kutegemea matumizi ya moja kwa moja ya virutubisho, wakati vipengele vingine vya ukuaji kama vile mwanga, nyuzi joto na maji viko katika hali inayofaa. Uwezo huu hautegemei kwenye wingi wa virutubisho kwenye udongo peke yake, lakini pia kwenye ufanisi wa kubadilisha virutubisho ndani ya duara la virutubisho shambani. Katika kubadilisha virutubisho, viumbe vya udongo vina jukumu muhimu. Huvunja vunja majani na sehemu nyingine zinazotokana na mabaki ya mazao shambani, mbolea ya kijani na matandazo na kuchangia katika kuongeza mabaki ya viumbe hai, ikiwemo na mboji, hazina ya virutubisho muhimu zaidi kwenye udongo. Viumbe hawa pia hutekeleza jukumu muhimu la kuhamisha mabaki ya viumbe hai kwenye udongo hadi hatua ya kuwa mfumo wa madini, ambayo yanaweza sasa kutumika na mimea. Viumbe vya udongo pia hulinda mimea dhidi ya magonjwa na kufanya udongo umeng’enyeke. Ni rahisi kufanya kazi kwenye udongo wenye rutuba, hunyonya maji ya mvua vyema na ni thabiti dhidi ya kujaa tope na mmomonyoko. Huchuja maji ya mvua na kutupatia maji safi ya kunywa. Huzimua (huzuia) tindikali, ambalo hupita kwenye hewa chafu na kutua juu ya udongo, na kuozesha kemikali zinazochafua mazingira kama vile viuatilifu haraka. Na mwisho japo pia ni muhimu, udongo wenye rutuba ni hazina ya ufanisi ya virutubisho na hewa ya kaboni (CO2 ). Kwa njia hii udongo wenye rutuba huzuia mlundikano wa virutubisho kwenye mito, maziwa na bahari na kuchangia katika kupunguza kupanda kwa joto duniani. Katika mazingira ya kilimo cha kibiolojia, rutuba ya udongo kimsingi ni matokeo ya michakato ya kibiolojia na sio virutubisho vya kikemikali. Udongo wenye rutuba uko katika mbadilishano ulio hai na mimea, hujiumba upya na una uwezo wa kujifufua. Sifa za kibiolojia zinaweza kuonekana katika shughuli za ubadilishaji zinazofanyika kwenye udongo, katika uwepo na dalili zinazoonekana za viumbe ndani yake. Jamii ya vijidudu iko thabiti na hufanya kazi katika muda stahiki. Katika mahusiano ya kiekolojia yanayojidhibiti yenyewe, wanyama, mimea na vijidudu wote hufanya kazi kwa manufaa ya wote. Ni jukumu la wakulima kuelewa ekolojia ya udongo hadi kufikia mahali ambapo wanaweza kujenga au kurudishia hali ya uwiano thabiti kwenye udongo. Kama udongo utakuwa hauleti mavuno mazuri mara kwa mara, wakulima wanapaswa kuchunguza sababu ya kufanya hivyo.  


 Sifa za udongo wenye rutuba

 Udongo wenye rutuba:

 a) una virutubisho vingi muhimu kwa ajili ya lishe ya msingi ya mmea (ikiwemo naitrojeni, fosfora, potasiam, kalsiam, magnesia na salfa kwa kupima virutubisho ndani ya udongo utawasiliana na mimi kwa namba za simu mwishoni
 b) una virutubisho vya kutosha vinavyohitajika kwa kiwango kidogo sana na mmea (ikiwemo boroni, kopa, chuma, zinki, manganizi, klorini na molibdenam);
 c) una kiasi stahiki cha mabaki ya viumbe hai kwenye udongo; 
d) una kipimo cha pH katika kiwango kinachofaa kwa ajili ya uzalishaji wa mazao (kati ya 6.0 na 6.8 pia kwa kupima pH wasiliana na mimi)
e) una muundo unaomeng’enyuka; 
f) uko hai kibiolojia; 
g) una uwezo mzuri wa kuhodhi maji na kutoa virutubisho


Kiasi stahiki cha virutubisho vya mmea 

UPIMAJI WA VIRUBISHO VYA UDONGO

Kuna aina 16 ya virutubisho muhimu ambavyo mimea huhitaji ili kukua vizuri. Kati ya elementi hizi 16 muhimu; haidrojeni, kaboni na oksijeni hupatikana kwa sehemu kubwa kutoka kwenye hewa na kwenye maji. Elementi nyingine muhimu hutoka ardhini na kwa ujumla husimamiwa na wakulima. Baadhi ya virutubisho hivi huhitajika kwa wingi katika tishu za mmea na huitwa ‘virutubisho vikubwa’. Virutubisho vingine vinahitajika kwa kiasi kidogo hivyo huitwa ‘virutubisho vidogo’. Virutubisho vikubwa vinajumuisha naitrojeni (N), fosfora (P) potasiam (K), kalsiam (Ca), magnezia (Mg) na salfa (S). Kati ya hizi N, P na K kwa kawaida huisha ardhini kwanza kwa sababu mimea inayahitaji kwa wingi kwa ajili ya ukuaji na maendeleo yao, hivyo hujulikana kama virutubisho vya msingi kupima virutubisho hivi wasiliana na mimi mwenyewe. Ni nadra kwa Ca, Mg na S kuwa kikwazo kwa ukuaji wa mmea, hivyo hujulikana kama virutubisho vya umuhimu wa pili. Pale ambapo udongo una asidi, chokaa mara nyingi huongezewa, ambayo ina kiasi kikubwa cha kalsiam na magnezia. Salfa kwa kawaida hupatikana katika mabaki yanayooza ya viumbe hai. Virutubisho vidogo ni: boroni (B), kopa (Cu), chuma (Fe), kloraidi (Cl), manganizi (Mn), molibdenam (Mo) na zinki (Zn). Kurejeshea mabaki ya viumbe hai kama vile mabaki ya mazao na majani ya miti ni njia bora ya kuipatia mimea inayokua virutubisho vidogo.


 Vitu vinavyowezesha mizizi kufyonza virutubisho kwenye Udongo

 a) Kwanza, udongo lazima uwe na unyevu wa kutosha kuruhusu mizizi ichukue na kusafirisha virutubisho. Wakati mwingine kuipatia mimea maji kutaondoa dalili za upungufu wa virutubisho.
b) Pili, kipimo cha kupima uasidi cha pH ya udongo lazima kiwe katika kiwango fulani ili virutubisho viweze kuachiwa kutoka kwenye punje za udongo. 
c) Tatu, nyuzi joto ya udongo lazima iwe katika kiwango fulani ili unyonyaji wa virutubisho uweze kutokea.
 d) Nne, virutubisho lazima viwepo karibu na eneo la mizizi ili mizizi iweze kuvifi kia. 

Kiwango cha nyuzi joto, pH na unyevu ni tofauti kwa aina tofauti za mimea. Kwa hiyo kihalisia virutubisho vinaweza kuwepo kwenye udongo, lakini visiweze kunyonywa na mimea. Ujuzi wa pH ya udongo, umbile asili na historia unaweza kuwa wa manufaa sana kwa kutabiri ni virutubisho gani vinaweza kuwa pungufu. Kwa upande mwingine, virutubisho vikizidi sana vinaweza kuwa sumu kwa mimea. Hii mara nyingi hushuhudiwa na dalili za mmea kuunguzwa na chumvi lakini ukipima udongo wako nitakuambia utumie mbolea gani zaidi na kwa kiasi gani kulingana na ukubwa wa shamba lako na zao unalolima kitaalamu zaidi. Dalili hizi hujumuisha majani kuwa ya kahawia pembezoni, ikitengwa na sehemu za kijani na mduara mdogo wa njano. Mwelekeo huu wa majani kuwa kahawia, ambao ni kuonyesha kifo cha majani, kuanzia kwenye ncha na kuendelea hadi shina la jani kupitia pembezoni mwa jani.

Udongo usio na asidi wala alikali (huru) 

KIFAA CHA KUPIMIA UDONGO
kipimo huru cha pH Kipimo cha udongo cha pH, ambacho huonyesha uasidi au ualikali, kinahusika zaidi katika jinsi virutubisho vinavyoweza kupatikana kwa urahisi kwenye udongo, ikijulikana kama uyeyushaji wa virutubisho. Katika bara la Afrika, takribani theluthi moja ya udongo una asidi au kuna uwezekano kuwa na uasidi na theluthi nyingine sio ya chumvi wala alikali, aina zote hizi ni vigumu kudhibiti. Mimea inatofautiana jinsi inavyoathiriwa na kiwango cha chini au juu cha pH. Mimea mingine huvumilia au hata kupendelea kiwango cha chini cha pH, mingine inapenda kiwango cha juu cha pH. Udongo wenye pH chini ya 6.5 ambao huweza kurekebishwa na chokaa unaweza kuchukuliwa kwamba ni udongo wenye asidi lakini lazima iwekwe kwa kiwango kinachohitaji , fuata ushauri kabla ya kuweka. Potasiam, kalsiam na Magnezia inapochuja kutoka kwenye udongo, udongo huwa na asidi. Hii inaweza kutokea kama kuna mvua nyingi (au maji ya umwagiliaji) ambayo huondoa virutubisho, au iwapo mbolea nyingi ya madini yenye naitrojeni itakapotumika. Katika udongo wenye asidi, mizizi ya mimea haikui kawaida kutokana na ayoni za sumu za haidrojeni. Fosforasi haiwezi kusafi rishwa na upatikanaji wake hupungua. Shughuli nyingi za viumbe rafiki kama bakteria wa spishi za Azatobacter na bakteria wanaotengeneza nundu kwenye mikunde pia huathirika kadri asidi inavyoongezeka katika mazingira ya asidi, bakteria huambisha naitrojeni kidogo zaidi na kuozesha mabaki kidogo ya viumbe hai yenye kiwango kidogo cha sumu, hivyo hupelekea virutubisho vichache kupatikana. Kuongeza chokaa au mboji yenye pH ya juu (8) kutasaidia kuzimua asidi na kuongeza pH, ili upatikanaji wa virutubisho uongezeke. Udongo wenye alikali hutengenezwa kutokana na mkusanyiko wa sodiam inayoweza kutumika na mimea na pH ya juu. Udongo unaomwagiliwa ambao haupenyezi maji vizuri unaweza kusababisha udongo wenye alikali. Katika maeneo ya pwani, kama udongo una kaboneti, kuingia kwa maji ya bahari kunasababisha udongo wenye alikali inayotokana na kulundikana kwa sodiam kaboneti. pH ya udongo wenye alikali inaweza kurekebishwa kwa kutumia jasi. Kwa kila milli-ikwivalenti 1 ya sodiam kwa gram 100 za udongo, takribani tani 1.7 za jasi huongezwa katika ekari ya ardhi. Kama mahitaji ni tani 3 kwa ekari, iwekwe mara moja. Iwapo mahitaji ni tani 5 au zaidi kwa eka, uwekaji ugawanywe sehemu 3. Kuongeza molasi au kupanda mazao ya mbolea ya kijani na kuzifukia shambani kunaweza kusaidia kurekebisha udongo wa alikali.


 Muundo unaomeng’enyuka

Mizizi ya mmea hupendelea udongo wenye muundo unaomeng’enyuka, kama mkate uliookwa vyema. Udongo kama huo unapitisha hewa vizuri na mizizi ya mmea inaweza kupenya kwa urahisi. Hii inaruhusu mizizi kukua kwa kwenda sehemu pana na chini zaidi ili kupata virutubisho zaidi vya kusaidia ukuaji mzuri. Mchanganyiko wa udongo pia ni kiashiria muhimu cha uwezekano wa kutumia udongo huo. Udongo ambao una chembechembe za kutosha inasemekana “unalimika vizuri”. Muundo mzuri wa udongo pia huchangia katika kupunguza mmomonyoko wa udongo wa juu, kwani maji hupenya kirahisi kuingia kwenye udongo na chembechembe za udongo huzuia matone ya mvua.


 Shughuli nyingi za kibiolojia

 Hata kama hatuvioni viumbe vingi vya udongo vikifanya kazi zao, viumbe wengi wa udongo ni muhimu sana kwa ubora na rutuba ya udongo. Vinachangia katika kubadili mabaki ya mazao na mbolea za asili na kufanya mboji, kuboresha afya ya mmea kwa kudhibiti wadudu na vijidudu vya magonjwa na kusaidia kuachia virutubisho kutoka kwenye chembe za madini. Shughuli nyingi za kibiolojia ni ishara ya udongo wenye rutuba. Viumbe vingi vya udongo hupendelea mazingira sawa na yale ya mizizi ya mimea: hali ya fukuto, nyuzijoto za wastani, hewa na mboji ni muhimu zaidi kwao. Vingi huathirika kwa urahisi na mabadiliko katika unyevu wa udongo na nyuzi joto. Shughuli yao kwa ujumla iko chini iwapo udongo ni mkavu, una maji mengi au joto kubwa. Iwapo udongo ni mgumu, umekauka au una mboji kidogo sana, unakuwa kama tofali la zege na viumbe wa udongo hawawezi kufanya kazi nzuri. Hata bakteria, pamoja na udogo wao, hawawezi kufanya kazi katika udongo uliokufa. Mzunguko mzuri wa hewa ndani ya udongo ni muhimu kwa maendeleo yao. Shughuli zinakuwa nyingi zaidi katika udongo wenye uvuguvugu na unyevu pale “chakula’” kinapopatikana.


 Kupima rutuba ya udongo

 Uchambuzi wa udongo

 Wakulima wanaweza wakagundua kwamba wakiweza kufanya uchambuzi wa udongo wao katika maabara ni jambo la manufaa linalowawezesha kufahamu habari zaidi kuhusu rutuba ya udongo wao. virutubisho vinyonywe kutoka kwenye udongo hutegemea vipengele vingi kwenye udongo, kama vile shughuli za kibiolojia. Wakati uchambuzi wa udongo unaweza kutoa majibu mazuri kwa udongo uliorutubishwa na mbolea za madini, shughuli nyingi za viumbe kwenye udongo katika udongo unaosimamiwa kwa kilimo hai huweza kupelekea upatikanaji mzuri zaidi wa virutubisho, hivyo kufanya matokeo ya uchambuzi kutofaa. Uchambuzi wa kikemikali wa udongo unaweza kutumika katika kuchambua kiwango cha asidi kwenye udongo (pH) au kwa kuchunguza upungufu au sumu zitokanazo na virutubisho kama vile Fosfora (P), Potasiam (K) au Zinki (Zn). Wakulima wa kilimo-hai wangependa kujua na kusimamia kiwango cha mboji kwenye udongo. Kwa udongo ambao umekuwa na matatizo kama vile mavuno machache kwa miaka mingi mfululizo, kufanya uchambuzi wa kawaida wa udongo kuangalia Fosfora, pH na mboji huweza kwa uhakika kuonyesha nini kifanyike ili kuboresha rutuba ya udongo. Uchambuzi wa kibiolojia wa viumbe vya udongo lazima ufanyike katika maabara zilizotengenezwa mahususi kwa ajili hiyo na ni zoezi ghali kidogo. Iwapo vipimo vya udongo vitatumika, wakulima wahakikishe kwamba vipengele husika vinachunguzwa na matokeo ya vipimo yanajadiliwa kwa kina na mtaalamu. Kwa wakulima wengi wa Tanzania, inaweza kuwa inafaa zaidi kutumia sepeto au jembe kwa ajili ya utambuzi na kuchimba udongo ili kuelewa vizuri zaidi aina zao za udongo na kuwekeza kwenye rutuba ya udongo kwa jumla. wataalamu wawahimize wakulima kuangalia shughuli za viumbe wa udongo ambao wanaozesha mimea na kuangalia hatma ya mimea baada ya kuozeshwa. Hii inaweza kuwa sehemu ya utambuzi kwa kutumia sepeto, lakini pia inaweza kuwa hatua ya kwanza kutambua udongo kama mfumo wa ikolojia ulio hai na unaofanya kazi.


 Changamoto zinazoambatana na mbolea za madini 

 Virutubisho katika mbolea za madini huyeyuka kwa urahisi, na hunyonywa kwa urahisi na mmea, lakini pia kuchujika nje ya udongo kwa urahisi (hasa naitrojeni). Inabidi mbolea hizi zitumike kwa uangalifu mkubwa ili zisiishie kuchafua chemchem au maji ya chini ya ardhi, ambayo husababisha matatizo ya kiafya kwa binadamu. Madini ya Naitreti yanayogundulika katika maji ya visima, kwa mfano hujulikana kusababisha kasoro katika mfumo wa chembe chembe nyekundu za damu (methaemoglobinaemia), ugonjwa unaojulikana pia kama “dalili za mtoto wa bluu” ambapo damu inakosa oksijeni kwa hiyo tunashauri wakulima kupima udongo ili kujua ni mbolea gani unatakiwa utumie, kwa kiwango gani? katika zao husika ili tuweze kuwa na ufanishi katika kilimo na utunzaji wa mazingira na vyanzo vya maji kwa ajili ya afya zetu(hasa maeneo ya pwani ambapo wanatumia sana maji ya visima)

No comments:

Powered by Blogger.