Header Ads

Breaking News
recent

HALI YA BIASHARA KWA SASA KATIKA SOKO LA MAWENZI MKOANI  MOROGORO.


   
 Mwenyekiti wa soko la Mawenzi mkoani morogoro  Ramadhani Mohamedi ametoa ufafanuzi juu ya hali ya biashara kwa kipindi cha  sasa  ambapo kumekuwa  na ongezeko kubwa la bei ya nyanya inayosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha  mashambani na kusababisha nyanya nyingi kuharibika.

 Ramadhani  Mohamedi amesema kuwa kuna baadhi ya bidhaa zilizo panda bei ususani zao la nyanya ambalo kwa kipindi hiki bei yake imekuwa ghali kutokana na nyanya nyingi kuozea shambani na kushwindwa kustahimili maji mengi yatokanayo na mvua.

Aidha,  ameongeza kwa kuwataka wafanya biashara wanaojishughulisha na uuzwaji wa bidhaa katika soko hilo kufuata taratibu na kanuni zilizo wekwa katika soko hilo ili kila mmoja aweze kunufaika kwa kufanya shughuli ya  biashara katika hali ya ufanisi na kushirikiana na viongozi  wa soko hilo.

Halikadhalika mmoja wa mfanya biashara katika soko hilo   Cosmas Pascal, ameongeza kwa kusema kuwa katika msimu huu  nyanya hulazimika kupanda bei kutokana na nyanya nyingi kuharibika shambani kutokana na wingi wa mvua  kunyesha na kupelekea nyanya nyingi kupasuka na nyingine kuoza hasa zikiwa bado shambani.

 Hata hivyo  kila mnunuzi wa bidhaa katika soko hilo anatakiwa kuto mkabidhi mzigo kijana yeyote asiye na vazi rasmi lenye namba ya utambulisho ili kuepukana na wingi wa matukio ya wizi yatokanayo na vijana wengi kujihusisha na kubeba mizigo ya mnunuzi na hatimaye kutokomea kusiko julikana.

No comments:

Powered by Blogger.